NA RUTH MBULA
MAAFISA wakiwemo wa kitengo cha GSU wamelizingira jengo la chama cha ushirika cha wahudumu wa bodaboda mjini Kisii na kuliwekea alama kuwa ni sehemu ya uhalifu.
Kamanda wa Polisi Kisii Bw Charles Kases amethibitisha kwamba kuna ambayo maafisa wanachunguza katika eneo hilo.
Hatua ya maafisa Ijumaa inajiri siku mbili tu baada ya maelfu ya wahudumu wa bodaboda kuzindua chama chao cha ushirika.
Jengo hilo liko nyuma ya jengo la Bunge la Kaunti ya Kisii.