• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 7:50 AM
Somalia, Afghanistan hatari zaidi kwa maisha ya watoto

Somalia, Afghanistan hatari zaidi kwa maisha ya watoto

Na MHARIRI

SOMALIA, Congo, Afghanistan na Syria zinaongoza katika orodha ya maeneo hatari zaidi ya kivita kwa watoto, Umoja wa Mataifa ulisema Jumatatu.

Mataifa hayo yanachangia karibu asilimia 60 ya visa vyote vya ukiukaji wa haki za watoto katika orodha yake ya mataifa ambapo dhuluma hizo zimekithiri.“Watoto hawawezi tena kuwa suala la mwisho la ajenda ya kimataifa wala kundi linalolindwa kwa kiasi kidogo zaidi miongoni mwa watu wote duniani.

”“Tunapaswa kuwapa watoto suluhisho. Tunahitaji amani, heshima kwa haki za watoto na demokrasia,” mwakilishi maalum wa watoto katika maeneo yenye ghasia, UN, Virginia Gamba, alisema Jumatatu.

Alisema visa vingi vya dhuluma mwaka uliopita vilihusu watoto kusajiliwa na kutumiwa vibaya na maafisa wa usalama na makundi ya wapiganaji pamoja na kuuawa na kulemazwa.“Tumehofishwa mno na ongezeko la kuwateka nyara watoto kwa asilimia 90 ikilinganishwa na miaka ya hapo mbeleni, ikiwemo kuongezeka kwa visa vya ubakaji na dhuluma nyinginezo za kingono kwa asilimia 70 ikilinganishwa na miaka ya awali,” alisema.

Zaidi ya watoto 3,200 walithibitishwa kutekwa nyara katika ghasia 2020, huku watoto wasiopungua 1,268 wakiwa wahasiriwa wa dhuluma za kingono, ilisema ripoti hiyo.Miongoni mwa mataifa mabaya zaidi, Gamba alisema “Somalia ilikuwa na visa vingi zaidi vya dhuluma dhidi ya watoto kufikia sasa,” vilivyotekelezwa hasa na magaidi wa Al-Shabaab.

Nchini Afghanistan, alisema wanamgambo wa Taliban walihusika kwa thuluthi mbili ya ukiukaji wa haki huku serikali na makundi ya wapiganaji yanayounga mkono serikali yakichangia vilivyosalia.Myanmar pia iliorodheshwa juu katika orodha hiyo ya ukiukaji uliokithiri wa haki ikiwemo idadi kubwa ya watoto wanaosajiliwa vitani na kutumika vibaya, huku Yemen ikiongoza kwa idadi kubwa ya watoto wanaouawa na kulemazwa.

Visa vya mashambulizi shuleni na hospitalini vilisalia kuwa juu mnamo 2020, vikifikia 856, hususan Afghanistan, Congo, Syria na Burkina Faso. ‘Elimu dhidi ya wasichana hasa ndiyo iliyolengwa,” alisema.Janga la Covid-19 lilifanya hali kuwa mbaya zaidi sawa na mambo mengine yote yaliyoathirika 2020.

Kwa mfano, kulingana na ripoti hiyo, matumizi ya shule na makundi ya wapiganaji yaliongezeka mwaka jana.Shule nyingi zilifungwa kwa muda kwa sababu ya janga la virusi vya corona hivyo kuzifanya kulengwa kirahisi, kugeuzwa makazi na kutumiwa na wapiganaji.

  • Tags

You can share this post!

Raila, Kalonzo wapeleka vita vyao Mt Kenya

‘Ushirika wa ODM, Jubilee moto wa kuotea mbali’