• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 5:50 AM
Tanzia: Afisa wa serikali ya Kilifi auawa kwa kudungwa kisu nyumbani

Tanzia: Afisa wa serikali ya Kilifi auawa kwa kudungwa kisu nyumbani

NA MAUREEN ONGALA

AFISA wa kike katika serikali ya Kilifi ameuawa kwa kudungwa na kifaa cha nyumbani leo Alhamisi.

Afisa Mkuu wa Uchumi wa Baharini Bi Rahab Karisa ametendewa unyama huo na mjakazi wake ambaye amemdunga kisu asubuhi na mwili wake tayari umepelekwa katika mochari ya Hospitali ya Rufaa ya Kilifi.

Maafisa wakiubeba mwili wa marehemu Bi Rajab Karisa aliyeuawa kwa kudungwa kisu nyumbani Mnarani, Kaunti ya Kilifi. Inadaiwa mfanyakazi wake wa nyunbani ndiye aliyetekeleza unyama huo. PICHA | MAUREEN ONGALA

Kamanda wa Polisi Kaunti ya Kilifi Bi Fatuma Hadi amethibitisha tukio hilo la kuhuzunisha.

“Kwa sasa majeraha yanayoenekana ni ya kisu lakini tunaendeleza uchunguzi na tutajua mengi baada ya mwili kufanyiwa upasuaji,” amesema kamanda Hadi.

  • Tags

You can share this post!

Beki Jurrien Timber aimarisha safu ya ulinzi kambini mwa...

Wanaharakati wakashifu tukio askari kujifanya mwanahabari...

T L