• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 3:23 PM
Wanahabari wa bungeni wachagua viongozi wapya

Wanahabari wa bungeni wachagua viongozi wapya

Na CHARLES WASONGA

CHAMA cha wanahabari wanaoripoti masuala ya bungeni (KPJA) Ijumaa kiliandaa uchaguzi wa viongozi wake wapya ambapo ripota wa gazeti la The Standard Moses Njagi alichaguliwa kuwa mwenyekiti.

Bw Njaji ambaye alipata kura 26 alifuatwa kwa umbali na ripota wa runinga ya Citizen Stephen Letoo aliyezoa kura nane. Wa tatu alikuwa mwenzao wa runinga ya KBC Kevin Wachira aliyepata kura tano pekee.

Bi Halima Osman, mwanahabari wa redio ya Baraka FM naye alichaguliwa bila kupingwa, kuwa naibu mwenyekiti katika uchaguzi huo ulioendeshwa katika majengo ya bunge, Nairobi.

Mwenyekiti mpya wa KPJA Moses Njagi (Standard) asema na mwenyekiti anayeondoka Gideon Keter (The Star). Picha/ Charles Wasonga

Wadhifa wa katibu mkuu nao ulivutia wagombeaji wawili; Bi Elizabeth Mutuku wa idhaa ya Kikristo, ATG Radio, na mwenzake Edward Kabasa, mtangazaji wa runinga ya KBC. Bi Mutuku alipata ushindi mkubwa kwa kujizolea kura 30 huku Kabasa akipata kura tisa.

Na wadhifa wa katibu mratibu ilimwendea James Murimi wa gazeti la The People Daily aliyepata ushindi kwa njia rahisi baada ya Hillary Mageka wa gazeti la Xnews kujiondoa kinyang’anyironi.

Baada ya kukamilika kwa zoezi hilo, lililosimamiwa na Afisa Mshirikishi wa Wanahabari Bungeni Washington Otiato, walioshindwa walikubali matokeo hayo, na kuwapongeza washindi huku wakiahidi kushirikiana nao kusukuma gurudumu la KPJA.

Kutoka kushoto: Ruth Njuguna (Redio Citizen), naibu mwenyekiti mpya Halima Osman (Iqra FM), mwenyekiti Moses NJagi (Standard), katibu mkuu mpya Elizabeth Mutuku (ATG Radio), mwenyekiti anayeondoka Gideon Keter (The Star), mwanachama Stephen Letoo (Citizen TV) na katibu mratibu James Murimi (The People Daily). Picha/ Charles Wasonga

“Pongezi mwenyekiti. Nimekubali kwamba ulikuwa na ushawishi mkubwa na kunishinda. Sasa tufanye kazi pamoja kwa manufaa ya KPJA,” Bw Letoo akamwambia Bw Njagi huku akimsalimia kwa furaha.

Bw Wachira naye alimpiga Njagi pambaja akimwambia, “Pongezi Kaka. Ushindi wako ni wa kweli. Sasa kazi kwako…sote tutashirikiana nawe kuhakikisha kuwa KPJA imefikia ufanisi.”

Bi Mutuku na Bw Kabasa nao walikumbatiana kwa furaha punde tu matokeo yalipotangazwa.

Katika hotuba yake Bw Njagi aliahidi kufanya kazi na wanahabari kutoka vyumba vyote vya habari ambao huripoti kutoka bunge huku akiwapongeza wenzake alioshindana nao.

Baadhi ya viongozi na wananchama walioshiriki uchaguzi wa Agosti 24, 2018. Picha/ Charles Wasonga

“Kwanza nawapongeza ninyi wanachama wote KPJA kwa kunipa heshima ya kuwa mwenyekiti wenu kwa kipindi cha mwaka mmoja ujao.

Naahidi kuwahudumia kwa bidii na moyo wa kujitolea na bila ubaguzi wote. Mimi sio bora zaidi kuliko wenzangu ambao niliwashinda… kwa hivyo nitashauriana nao kila wakati,” akasema Bw Njagi huku akishangiliwa na wanachama.

Kwa upande wake, mwenyekiti anayeondoka Bw Gedion Keter wa gazeti la The Star aliwapongeza maafisa wapya waliochaguliwa na kuahidi kuwaelekeza ili waweze kuwahudumia wanachama ipasavyo kulingana na katiba ya chama hicho.

Washindani wa wadhifa wa katibu mkuu Bw Edward Kabassa (KBC TV) amkumbatia Bi Elizabeth Mutuku aliyemshinda kwa kura 21. Picha/ Charles Wasonga

“Ni furaha yangu kwamba uchaguzi wa Ijumaa umeendeshwa kwa njia nzuri na wagombea wote wameridhishwa na matokeo. Napongeza wenzetu walioshinda, wakiongozwa na Bw Njagi, na kuahidi kuwa nitawapa ushauri wowote ambao watahitaji. Nawahongera pia wale walioshindwa kwa kuonyesha ukomavu,” akasema.

Mojawapo ya malengo ya KPA ni kushirikiana na asasi ya bunge kuwawezesha wanahabari kupata habari, kuhusu shughuli za bunge kwa njia faafu.

Chama hicho pia kinashirikiana na mashirika mbalimbali kwa lengo la kutoa mafunzo ya kila mara kwa wanahabari ili waimarishe utendakazi wao.

Kutoka kushoto: Naibu mwenyekiti Halima Osman (Iqra FM), mwenyekiti Moses NJagi (Standard), katibu mkuu Elizabeth Mutuku (ATG Radio) na katibu mratibu James Murimi (The People Daily). Picha/ Charles Wasonga

Viongozi na wanachama wa KPJA pia huandamana na Spika wa Bunge Justin Muturi, wabunge na maafisa wa bunge katika ziara zao nje ya nchi kwa shughuli mbalimbali muhimu za kikazi.

Kwa mfano, wiki iliyopita mwenyekiti anayeondoka Bw Keter na mwanachama John Nyaga (mpiga picha wa runinga ya K24) waliandamana na Spika Muturi katika ziara ya kikazi jijini Gaborone nchini Botswana.

Bw Muturi alikuwa amehudhuria Kongamano la 46 la Shirikisho la Mabunge ya Mataifa Wanachama wa Jumuiya Madola, ukanda wa Afrika (CPA-A).

Spika Muturi alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati Kuu ya shirikisho hilo wakati wa kongamano hilo ambalo lilidumu kwa siku kumi.

Kutoka kushoto: Waliowania uenyekiti Kevin Wachira (KBC), Stephen Letoo (Citizen TV), Moses Njagi (Standard) na ajenti wa Bw NJagi, Grace Njihia (Kameme TV). Picha/ Charles Wasonga

 

Orodha Rasmi ya Wanachama wa KPJA 2018

1. Edward Kabassa, KBC TV

2. Crane Senteman, Ebru Tv

3. Laban Wanambisi, Capital FM

4. Geofrrey Mosoku, The Standard

5. Josphine Karani, Bunge TV

6. Simon Macharia, Inooro TV

7. Stephen Letoo, Citizen TV

8. Anthony Mwangi, The People Daily

9. Mercy Mwai, The People

10. Carol Korir, Baraka Fm

11. Lucy Kilalo, Taifa Leo/ Taifa Jumapili

12. Lynette Igadwa, Business Daily

13.  Ruth Njuguna, Radio Citizen

14. Grace Njihia, Kameme TV

15. Chris Nyamuta, Baraka FM

16. Kennedy Mureithi, NTV

17. Grace Ndungu, Ebru TV

18. David Mwere, Daily Nation

19. Elizabeth Mutuku, ATG Radio

20. Dina Ondari, The People Daily

21. Jane Goin, K24 TV

22. Patrick Amimo, KTN News

23. John Nyaga, K24

24. James Murimi, The People Daily

25. Charles Wasonga, Taifa Leo/Taifa Jumapili

26. Glady Mungai, Inooro Tv

27. Joseph Njane, Redio Citizen

28. Ibrahim Oruko, Daily Nation

29. Hillary Mageka, Xnews

30. James Mbaka, The Star

31. Boniface Okendo, The Standard

32. Moses Njagi, The Standard

33. Edwin Obuya, Redio Citizen

34. Aaron Kinamaso, ATG Redio

35. Halima Osman, Iqra FM

36. Zainab Ismael, Iqra FM

37. Dancan Khaemba, KTN News

38. Chris Thairu, KTN News

39. Cecilia Wakesho, KTN News

40. Eric Munene, Inooro Fm

41. Daniel Psirmoi, The Standard

42. Samwel Owino, Daily Nation

43. Kevin Wachira, KBC TV

44. George Okachi, Ebru TV

You can share this post!

Madereva waliokwepa ushuru wakamatwa mpakani

Kofi Annan kuzikwa nchini Ghana Septemba 13

adminleo