• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 4:36 PM
ICC yamtupa Bemba jela mwaka mmoja

ICC yamtupa Bemba jela mwaka mmoja

MASHIRIKA na PETER MBURU

HAGUE, UHOLANZI

MAHAKAMA ya Kimataifa kuhusu Kesi za Jinai Jumatatu ilimfunga kwa mwaka mmoja gerezani aliyekuwa naibu wa Rais Congo Jean-Pierre Bemba kwa kuwahonga mashahidi katika kesi ya awali, ambayo ilimfanya akatazwe kuwania Urais.

Majaji hao walimfunga Bemba kwa kipindi hicho, hata baada yao kulalamika mbeleni kuwa kipindi hicho kilikuwa kidogo sana, huku upande wa mashtaka ukiwa ulikuwa umeitaka korti kumfunga kwa kipindi cha juu zaidi kisheria cha miaka mitano.

 Mwanasiasa huyo wa miaka 55 ambaye alikuwa amekuwa kiongozi wa waasi Congo mbeleni alikuwa ameachiliwa na mahakama ya ICC mbeleni kwa mashtaka ya kivita na dhuluma za jinai dhidi ya binadamu alipokata rufaa miezi mitatu iliyopita.

“Korti inamhukumu Bw Bemba kwa jumla ya miezi 12 jela. Baada ya kupunguza muda kutokana na muda aliokaa ndani mbeleni, korti inachukulia muda huo kama aliotumikia kifungo,”akasema Jaji Bertram Schmitt.

Aidha, Bemba alipigwa faini ya Euro 300,000.

Kifungo chake hicho kilitokana na mashtaka kuwa alipokuwa akifanya kesi ya vita na dhuluma dhidi ya binadamu aliwahonga mashahidi na kuwaeleza mashahidi 14 cha kusema kortini.

Alifungwa kifungo sawia Machi baada ya kupatikana na hatia hiyo, akiwa pamoja na 14 wenzake, lakini majaji wa mahakama ya rufaa ICC wakarejesha kesi jikoni kwa madai kuwa kifungo hicho cha mwaka na faini ya Euro 300,000 kilikuwa kidogo mno.

Lakini Jumatatu, Jaji Schmitt alisema kuwa kifungo cha muda mrefu sana kinachoruhusiwa kisheria hakifai katika kesi hiyo.

Kifungo hicho sasa kimekuwa pigo kwa Bemba ambaye amekuwa na malengo ya kuongoza taifa hilo lililokumbwa na ghasia kwa miaka mingi.

You can share this post!

Kisa cha maiti za watoto kupatikana kwa maboksi Pumwani...

Shabiki wa Zoo aliyewatisha wapinzani kwa bastola taabani

adminleo