• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 6:55 AM
ODM yapanga kumvua Obado ugavana

ODM yapanga kumvua Obado ugavana

Na Elisha Otieno

MASAIBU yanazidi kumkumba Gavana Okoth Obado, baada ya ODM kuanzisha kampeni ya kuwataka madiwani wa Kaunti ya Migori kupiga kura ya kumwondoa uongozini.

Mwenyekiti wa chama hicho Kaunti ya Migori, Bw Philip Makabong’o anasema kuna majadiliano ili ikiwezekana, Bw Obado aondolewe ofisini.

“Madiwani wana siku 14 kumwondoa gavana huyo, la sivyo chama kichukue jukumu hilo. Kwa hakika ODM tuko katika makini kuhusu jambo hili,” aliwambia wanahabari.

Bw Makabong’o alisema ODM kina mbinu kadhaa kitakazotumia kutekeleza jambo hilo, kwa kuwa kinaamini kuwa gavana ameshindwa kufikia matakwa ya maadili ya uongozi.

“Tuna madiwani zaidi ya 40 wa ODM kati ya madiwani wote 57. Mbali na kesi ya uhalifu inayomkabili mahakamani, Bw Obado si mwaminifu kwa uongozi wa chama,” akasema.

Gavana huyo atarejeshwa kortini Jumatano wiki hii kujua kama atapewa dhamana kuhusiana kesi ya mauaji ya mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Rongo, Sharon Otieno.

 

You can share this post!

Raila atasalia kwa siasa licha ya kuteuliwa AU –...

Wanafunzi sasa kujiunga na vyuo vya ualimu kwa alama ya D+

adminleo