• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 10:08 PM
Waziri kujibu mashtaka kwa kumwondoa Atwoli NSSF

Waziri kujibu mashtaka kwa kumwondoa Atwoli NSSF

Na BERNARDINE MUTANU

Waziri wa Leba Ukur Yatani ana hadi Jumatano kujibu mashtaka yaliyowasilishwa mahakamani na COTU kuhusiana na hatua yake ya kutomteua tena Francis Atwoli katika bodi ya Hazina ya Malipo ya Uzeeni (NSSF).

Washtakiwa walitakuwa na Jaji Onesmus Makau Jumatatu kuwasilisha majibu kabla ya kusikizwa kwa kesi hiyo Jumatano.

Chama hicho cha wafanyikazi kinataka mahakama kusimamisha bodi ya NSSF kufanya mikutano yoyote kabla ya kuchapishwa jina la Atwoli katika gazeti rasmi la serikali.

COTU ilienda mahakamani wiki jana kwa kusema kukataa kuteuliwa kwa Atwoli ni kinyume cha Sheria ya NSSF, 2013.

Kulingana na COTU, ikiwa NSSF itafanya mkutano wowote, lazima wafanyikazi na waajiri wao wawakilishwe.

Kupitia kwa wakili wake Okweh Aichiando, COTU ilisema mkutano wowote wa NSSF bila COTU ni kinyume cha matakwa ya wafanyikazi, wachangiaji wakubwa zaidi wa hazina hiyo.

You can share this post!

KRA yalemewa na Google kortini kuhusu udukuzi wa mitambo

Fifa kuipa Kenya Sh100 milioni kuinua soka ya vipusa

adminleo