• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 9:15 PM
Msemaji wa Machar kunyongwa kwa kujaribu kupindua serikali ya Sudan Kusini

Msemaji wa Machar kunyongwa kwa kujaribu kupindua serikali ya Sudan Kusini

MSEMAJI wa kiongozi wa waasi Riek Machar, Bw James Gatdet Dak azogwa na mawazo baada ya kuhukumiwa kunyongwa kwa kutekeleza uchochezi na kujaribu kupindua serikali ya Sudan Kusini. Picha/ Maktaba

Na MASHIRIKA

JUBA, SUDAN KUSINI

MSEMAJI wa kiongozi wa waasi Riek Machar, amehukumiwa kunyongwa baada ya kupatikana na hatia ya kutekeleza uchochezi na kujaribu kupindua serikali.

James Gatdet Dak alisafirishwa kwa nguvu na Kenya kwenda Sudan mnamo Novemba 2016, hatua iliyokosolewa na Umoja wa Mataifa (UN) na makundi ya kutetea haki za kibinadamu kuwa ilikiuka sheria za kimataifa.

Mahakama Kuu jijini Juba ilimhukumu Gatdet adhabu ya kifo pamoja na kifungo cha miaka 21 gerezani, Jumatatu, kwa kujaribu kupindua serikali ya Rais Salva Kiir.

Wakili wa Gatdet, Monyluak Alor Kuol alipinga hukumu hiyo huku akisema kuwa ilikiuka mkataba wa amani uliotiwa saini Desemba uliotaka wafungwa wote wanaozuiliwa kwa sababu za kisiasa kuachiliwa huru.

“Nimesikitika sana. Kesi za kisasa hazifai kufanyika kwa sasa,” akasema Kuol.

Gatdet alishtakiwa pamoja na William John Endley, raia wa Afrika Kusini, ambaye alikuwa mshauri wa Machar.

Kesi dhidi ya Endley inaendelea na mahakama inatarajiwa kutoa uamuzi mwishoni mwa mwezi huu.

 

You can share this post!

Kituo cha redio cha Kikristo chafungwa kudunisha wake

Utafiti: Wasiotafuna mlo vyema hatarini kunenepa kupindukia

adminleo