Habari za Kitaifa

Mtoto Ian aliyeibwa na yaya apatikana

June 7th, 2024 1 min read

NA MERCY MWENDE

MTOTO Ian Kariuki aliyekuwa ameibiwa na yaya kutoka nyumbani kwao Kiamwathi, Nyeri, amepatikana.

Mnamo Ijumaa, mtoto huyo aliungana na familia yake.

Wakati alipelekwa katika hospitali ya Equity Afia mjini Nyeri kwa gari la polisi, shangwe na vigelegele vilisikika akichukuliwa na mama yake Bi Joyce Wanjeri na babake Bw Bw Michael Kariuki.

Polisi walisema kuwa wenyeji walipata mtoto huyo katika msitu wa Tetu ambapo amekuwa akiishi na yaya huyo, Bi Jane Nyambura mwenye umri wa miaka 46.

Soma Pia: Yaya atoweka na mtoto wa umri wa mwaka mmoja Nyeri

Inadaiwa wamekuwa wakiishi msituni humo kwa muda wa wiki moja.

Ian mwenye umri wa mwaka mmoja na miezi saba, alitoweka mnamo Mei 31, 2024.