• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 6:50 PM
Muafaka umeimarisha utalii nchini – Ripoti

Muafaka umeimarisha utalii nchini – Ripoti

Na BERNARDINE MUTANU

Sekta ya utalii imeimarika kwa asilimia kubwa ikilinganishwa na mwaka wa 2017.

Mapato katika sekta hiyo yaliimarika kwa asilimia 31.2 mwaka wa 2018 kulingana na data mpya kutoka kwa Wizara ya Utalii na Wanyamapori.

Wizara hiyo ilitangaza mapato ya Sh157.38 bilioni kutoka Sh119.0 bilioni mwaka wa 2017. Kulingana na serikali, mapato hayo yaliimarika kutokana na kuimarika kwa usalama nchini na hatua ya serikali kudhibiti ugaidi.

Pia hali dhabiti ya kisiasa baada ya muafaka imepelekea kuongezeka kwa watalii nchini, ilisema wizara hiyo.

Sekta hiyo imeshuhudia ongezeko la asilimia 68 ya watalii kutoka nje ya nchi hadi 2.025 milioni kutoka 1.46 milioni mwaka wa 2017.

Utalii wa humu nchini uliimarika kwa asilimia 9.03 kutoka siku 3.64 hadi 3.97 kiwango cha vitanda vilivyohifadhiwa.

Idadi ya watalii kutoka Afrika ilipita watalii kutoka kwingineko kwa asilimia 40.76 (825,489).

Watalii kutoka Tanzania walikuwa ni 212,216 ilhali wale kutoka Uganda walikuwa 204,082.

Waliotoka Uropa walikuwa 611,969 au asilimia 30.33 (Ujerumani 48,189 Ufaransa, Uhispania 25,027 na Sweden 22,028).

Watalii kutoka Marekani nchi walikuwa ni asilimia 11.12 au 225,157.

You can share this post!

Kero mtoto kubakwa kisha kukatwa sehemu nyeti kwa wembe

Sonko kutaja naibu huku waziri akidai kugeuzwa mke

adminleo