Habari za Kitaifa

Washukiwa 13, akiwemo mshukiwa wa mauaji ya Kware wametoroka rumande

August 20th, 2024 1 min read

WASHUKIWA 13, akiwemo mshukiwa wa mauaji ya Kware Collins Jumaisi, wametoroka kutoka Kituo cha Polisi cha Gigiri, Kamanda wa Polisi Nairobi, Bw Adamson Bungei, amethibitisha.

Bw Bungei alieleza  kuwa washukiwa wengine 12 waliotoroka  mwendo wa saa tisa usiku, ni raia wa Eritrea, wenzao wawili wakisalia kituoni humo.