Habari za Kitaifa                                                
                                            
                                        Washukiwa 13, akiwemo mshukiwa wa mauaji ya Kware wametoroka rumande
 
                                                    
                                                        Aliyekuwa Mkuu wa Polisi Nairobi, Bw Adamson Bungei. PICHA|MAKTABA                                                     
                                                WASHUKIWA 13, akiwemo mshukiwa wa mauaji ya Kware Collins Jumaisi, wametoroka kutoka Kituo cha Polisi cha Gigiri, Kamanda wa Polisi Nairobi, Bw Adamson Bungei, amethibitisha.
Bw Bungei alieleza kuwa washukiwa wengine 12 waliotoroka mwendo wa saa tisa usiku, ni raia wa Eritrea, wenzao wawili wakisalia kituoni humo.