Shangazi Akujibu

SHANGAZI AKUJIBU: Majukumu yanilemea

Na SHANGAZI November 28th, 2025 Kusoma ni dakika: 1

SWALI: Hujambo shangazi. Nilianza kazi miezi michache iliyopita. Nilipolipwa mshahara wa kwanza, bili za nyumba zilimeza pesa zote. Naona heri niache kazi nirudi niishi na wazazi. Nipe ushauri.

Jibu: Sioni kama hatua hiyo itakusaidia. Usirudi kuishi na wazazi. Endelea na kazi ili ujifunze kujitegemea. Baada ya muda mambo yataanza kunyooka.

IMETAYARISHWA NA WINNIE ONYANDO