Habari

Sehemu ya barabara ya Uhuru kufungwa

Na HILLARY KIMUYU February 7th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

MAMLAKA ya Barabara Kuu Nchini (KeNHA) imetangaza kufungwa kwa muda kwa sehemu ya Barabara ya Uhuru kati ya mzunguko wa Chuo Kikuu cha Nairobi na mzunguko wa Westlands kwa kipindi cha wiki moja ili kupisha ukarabati.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Ijumaa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa KeNHA, Bw Luka Kimeli, barabara hiyo itakuwa ikifungwa kila usiku kuanzia saa nne usiku hadi saa kumi na moja alfajiri, kuanzia Februari 6 hadi Februari 13, 2026.
“KeNHA inawaarifu wananchi kuwa sehemu ya Barabara ya Uhuru kati ya mzunguko wa Chuo Kikuu cha Nairobi na mzunguko wa Westlands itafungwa kwa muda kila usiku kuanzia Ijumaa, Februari 6 hadi Ijumaa, Februari 13, 2026 kati ya saa 10:00 jioni na saa 5:00 asubuhi. Hatua hii ni kuwezesha kazi za matengenezo ya barabara,” alisema Bw Kimeli.
Madereva wanaoelekea Barabara ya Uhuru na Barabara ya Chiromo kuelekea Nakuru wametakiwa kutumia njia mbadala. Njia hizo ni pamoja na Barabara ya Nyerere, Arboretum Drive, Westlands Ring Road na Barabara ya Nairobi Expressway.