Shangazi Akujibu
SHANGAZI AKUJIBU: Nashuku ataniacha sababu sijamzalia
Mwanamke mjamzito. Picha|Maktaba
SWALI: Salamu Shangazi. Nimekuwa katika ndoa kwa miaka mitatu. Tatizo ni kuwa nimeshindwa kabisa kupata mtoto. Mume wangu anapenda watoto sana na nahofia ataniacha. Nifanyeje?
Jibu: Kumekuwa na dhana potovu kuwa shida ya kutopata watoto ni ya wanawake pekee. Wanaume pia huwa na shida hiyo. Kama hamjapimwa hospitalini ni muhimu mfanye hivyo ili mjue kiini cha tatizo hilo na iwapo linaweza kutibiwa.
IMETAYARISHWA NA WINNIE ONYANDO