Shangazi Akujibu

SHANGAZI AKUJIBU:Simpendi kabisa na amekazana anataka kunioa

Na SHANGAZI February 6th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

SWALI: Kwako shangazi? Nina mpenzi na anataka kunioa. Sina shaka tunapendana kwa dhati na sijawahi kuona ubaya wowote wake kwa miaka miwili ambayo tumekuwa pamoja. Lakini nahisi moyoni kuwa hatuwezi kuishi pamoja kama mume na mke. Nimechanganyikiwa, nishauri.

Jibu:Mapenzi na ndoa ni mambo mawili tofauti. Ndoa ni zaidi ya mapenzi. Licha ya mapenzi uliyo nayo kwa mwanamume huyo, yamkini moyo wako umeona udhaifu wake fulani ingawa huwezi kuutambua kwa sasa. Nakushauri ufuate moyo wako. Mwambie ukweli

IMETAYARISHWA NA WINNIE ONYANDO