Habari
Ujenzi wa makavazi ya Raila kuchukua miezi miwili
Waziri wa Ulinzi Soipan Tuya na Kinara wa ODM Oburu Oginga wakati wa uzinduzi wa ujenzi wa maziara ya Raila. PICHA|ALEX ODHIAMBO
WAZIRI wa Ulinzi Soipan Tuya amesema kuwa Kangó Ka Jaramogi alikozikwa marehemu Raila Odinga kumefungwa kwa miezi miwili kwa umma ili kuruhusu ujenzi wa maziara.
Bi Tuya, Kiongozi wa ODM Dkt Oburu Oginga, Raila Jnr, pamoja na Waziri wa Vyama vya Ushirika Wcliffe Oparanya na Naibu Gavana wa Kisumu Mathews Owili jana walizindua ujenzi wa maziara hayo ambayo yatafanywa na jeshi.
Bi Tuya alisema ujenzi huo utakuwa wa hadhi ambayo inastahiki sifa za marehemu Bw Odinga huku akihakikishia familia ya Jaramogi kuwa mradi huo utakamilika kabla ya maadhimisho ya mwaka mmoja tangu mauti ya kigogo huyo wa siasa za upinzani.