Mastaa wa Rangers walivyogeuza gym kuwa danguro
IMEFICHUKA kwamba baadhi ya masogora wa Rangers wamekuwa wakitumia vyumba vya hoteli vilivyotengewa wachezaji wenye majeraha kufanyia mazoezi ya viungo vya mwili kuendeleza michepuko!
Daktari wa klabu hiyo ya Scotland amesimamishwa kazi kutokana na madai hayo ya kushtua. Kwa mujibu wa wadadisi wa mambo ya ndani kambini mwa Rangers, hoteli moja inayotumika sana kwa ajili ya shughuli hizo iko Uingereza.
Kashfa hiyo ya ngono ilifichuliwa baada ya mke wa sogora mmoja wa Rangers kupata ithibati ya kuchepuka kwa mumewe.
Mke huyo aliwasiliana na uongozi wa Rangers baada ya kugundua udanganyifu wa mpenzi wake.
Hiyo ilichochea mtaalamu wa masuala ya mazoezi ya viungo vya mwili kambini mwa Rangers kusimamishwa kazi.
Haijulikani ni nyota wangapi hasa wamekuwa wakitumia vyumba hivyo kwa ajili ya michepuko na jambo hilo limefanyika kwa muda gani.
Kwa mujibu wa gazeti la The Sun, idadi kubwa ya wachezaji wa Rangers wamekuwa wakitumia vyumba vya hoteli zao mbalimbali nchini Uingereza kuburudishwa na wanawake.
Chanzo kimoja kilisema: “Kashfa hiyo ilifichuliwa kabla ya Krismasi ya mwaka jana na imesababisha dhoruba kubwa kikosini. Inashangaza kuwa vyumba vya wachezaji wanaoguza majeraha kufanyia mazoezi vinageuzwa kuwa madanguro.”
Mnamo 2019, aliyekuwa nyota wa Rangers Alfredo Morelos, aliweka ndoa kati yake na mkewe Yesenia katika hatari ya kuvunjika baada ya kunaswa na kamera akimwingiza demu raia wa Colombia katika chumba cha hoteli yake kisiri.
Mshambulizi huyo aliyekuwa na umri wa miaka 23 wakati huo alitumia chumba hicho kuponda raha na mwanamitindo huyo aliyetambuliwa kuwa Marian Cardenas.
Aidha, mnamo 2024 fowadi mwingine wa Rangers, Fashion Sakala, alifumaniwa hotelini akidokoa tunda la kimada wake Linnety Kaoma bila ya mkewe, Violet Zulu, kujua.