Kalameni alimwa na mkewe kwa kuleta nyumbani samaki aliyenunuliwa na kimada wake
MWISHO WA LAMI, Mombasa
POLO apewa kichapo kikali baada ya mkewe kugundua kuwa samaki aliyemletea nyumbani alikuwa amenunuliwa na mpango wa kando.
Jamaa aliingia akiwa amebeba mfuko wa nailoni kwa kujiamini, akitangaza kuwa kungekuwa na chajio spesheli.
Lakini hata kabla ya jiko kuwashwa, swali moja lilivunja utulivu.Huyu samaki ametoka wapi? mkewe aliuliza kwa sauti ya kawaida lakini yenye uzito.
Jamaa alijibu kwa haraka kuwa alikuwa amenunua mwenyewe.
Hata hivyo, bahati haikuwa upande wake kwani ushahidi ulikuwa tayari umefika.
Rafiki wa mkewe alimwona mpango wa kando wa jamaa mwenye pesa akimnunulia samaki huyo.
Mkewe alimchukua kwa mkono mmoja na kabla jamaa hajamaliza sentensi yake ya pili ya kujitetea, akamtwanga mgongoni huku akifoka.