Habari za Kaunti

Kaunti yampa mfugaji kuku ilani ya usafi baada ya malalamishi kuhusu uvundo, nzi

Na KNA June 23rd, 2026 Kusoma ni dakika: 1

MAAFISA wa afya ya umma wa Kaunti ya Kwale wametoa ilani ya siku 28 kwa wasimamizi wa shamba la kufugia kuku lililo katika kijiji cha Kiteje, Kaunti Ndogo ya Matuga, kushughulikia harufu mbaya iliyojaza nzi.

Afisa wa Afya ya Umma wa Matuga, Bw Vincent Mosomi, alisema serikali ya kaunti iliingilia kati baada ya wakazi kulalamika kuwa hali hiyo imeathiri afya na maisha yao.

Alibainisha kuwa shamba hilo, ambalo lina karibu kuku 9,000 wa kutaga, linakabiliwa na changamoto za kushughulikia uchafu, akiongeza kuwa nzi hao ni tishio kwa afya ya umma kwa vile wanaweza kusambaza magonjwa kama vile kipindupindu.

Mwekezaji alishauriwa kutumia mbinu endelevu za usimamizi wa taka, ikiwemo kutafuta njia za kubadilisha taka za kuku kuwa gesi ya kawi, huku ikitekeleza hatua za haraka za kudhibiti harufu na nzi.

Wasimamizi wa shamba hilo walikiri kupokea malalamiko na kusema tayari wameanza kuchukua hatua za kuboresha hali.