Waomba kesi ya mauaji ya Baby Pendo isitishwe
MAKAMANDA wanne wa polisi wanaoshtakiwa kwa mauaji ya Baby Samantha Pendo na watu wengine 34 wakati wa ghasia za baada ya uchaguzi wa 2017 mjini Kisumu wanaomba mahakama kuu itamatishe kesi inayowakabili wakidai ushahidi hauthibitishi makosa waliyofanya.
Mabw John Chengo Masha, Linah Kogey, Cyprine Robi Wankio na James Rono wameomba mahakama kuu isitishe kwanza kusikizwa kwa kesi dhidi yao kusubiri uamuzi wa ombi lao.
Makamanda hao wameshtakiwa kwa mauaji ya watu 35 akiwamo Baby Pendo, ubakaji na dhuluma za binadamu kinyume cha sheria za kimataifa zinazotetea binadamu.
Katika ombi hilo makamanda hao wanaomba mahakama iharamishe mashtaka mapya waliyoshtakiwa Mei 2025 wakidai “hakuna ushahidi wowote wa kuthibitisha walitekeleza uhalifu wowote.”
Makamanda hao wanadaiwa walisita kuzima polisi waliokuwa wanazima ghasia hizo kutotenda uhalifu.
Walalamishi hao wanadai sheria inamtaka Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP) kuhakikisha kwamba kuna ushahidi wa kutosha kabla ya mshukiwa yeyote kufunguliwa mashtaka.
Na wakati huo huo mahakama imeelezwa DPP hajawakabidhi washtakiwa nakala zote za ushahidi.
Mahakama kuu ilimwagiza DPP awakabidhi washtakiwa nakala zote za mashahidi katika muda wa siku 30.
Jaji anayesikiza kesi alisema endapo DPP hatakuwa amewakabidhi washtakiwa nakala zote za mashahidi hatakuwa na budi kusikiza ombi la kufutiliwa mbali kwa kesi hiyo.
Makamanda hawa wanasema ni takriban miaka 10 na kesi hiyo ingali kuanza.
Kesi dhidi ya makamanda hawa wa polisi ulifanywa na mamlaka huru ya kusimamia polisi.