Kioja mtaani baada ya msupa kupatikana na mizoga ya paka
MASII, MACHAKOS
MWANADADA mmoja katika mtaa huu amegeuka gumzo miongoni mwa majirani baada ya kudaiwa kupatikana na vitu vya kutatanisha vinavyohusishwa na uchawi.
Kisa kilianza mizoga kadhaa ya paka ilipopatikana karibu na njia ya kuelekea kwake katika mazingira yasiyoeleweka na polo mmoja akadai alimuona akichimba kitu nyuma ya nyumba usiku.
Makalameni wa mtaa walipochunguza walipata chupa zilizojaa vitu visivyojulikana, nywele na vipande vya nguo.
Mwanamke huyo alikanusha madai ya uchawi lakini akakiri kujikinga na watu wenye wivu.
Hata hivyo, majirani wanataka uchunguzi muhususi wa suala hilo.