Habari

Ruto apanua kikosi chake Ukambani kukabili Kalonzo

Na PIUS MAUNDU July 19th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

MAPAMBANO ya kisiasa ya kuwania takriban kura milioni mbili za Ukambani yamepamba moto baada ya Rais William Ruto kupanua orodha ya washirika wake katika eneo hilo kuelekea uchaguzi mkuu wa 2027.

Katika mkutano uliofanyika Ikulu Ijumaa, Rais Ruto aliwatambulisha aliyekuwa Mkuu wa Wafanyakazi Ikulu Nzioka Waita na aliyekuwa mwenyekiti wa Bodi ya Chuo cha Mafunzo ya Matibabu Kenya (KMTC) Prof Phillip Kaloki kama miongoni mwa viongozi watakaoimarisha chama cha UDA Ukambani.

Rais pia alimtangaza Prof Kaloki kuwa mgombea wa UDA wa ugavana wa Makueni, huku mkuu wa Mpango wa Kitaifa wa Kudhibiti Ukimwi na Magonjwa ya Zinaa (NASCOP), Dkt Andrew Mulwa, akitajwa kuwa mgombea wa useneta.

“Tutasimamisha wagombea katika nafasi zote nchini,” alisema Rais Ruto.

Aliwataka wakazi wa Ukambani kumuunga mkono mwaka ujao.