Mke aduwaa mume kugeukia makahaba kutafuta faraja baada mamake kuaga dunia
MWANADADA mmoja analalamikia ndoa yake baada ya mumewe kutumia pesa kwa makahaba kufuatia kifo cha mamake.
Kulingana naye, ameumia sana kihisia na tabia ya mumewe imeyumbisha imani aliyokuwa nayo kwake.
Asema mumewe alikiri alitumia pesa nyingi kwa wanawake hao huku akidai walimpa faraja alipokuwa akipitia kipindi kigumu kumpoteza mamake.
Hata hivyo, kinachomsumbua zaidi ni kwamba, mumewe anataka maisha yaendelee kana kwamba hakuna kilichotokea.
Anasema hawezi kusahau kwa urahisi usaliti huo, na anahisi kudharauliwa na kutothaminiwa.
“Anataka nijifanye kama kila kitu kiko sawa, lakini moyo wangu umeumia,” alisema.
Hii imemuacha njia panda, akijiuliza iwapo aendelee na ndoa hiyo au aondoke ili kulinda heshima na amani yake ya ndani.