VITUKO VYA MASTAA: Kahaba aapa kutofungua ‘duka’ hadi kocha wa kikosi apigwe kalamu
DANIELLA Chavez ameapa kutopakia tena picha na video za uchi wake kwenye jukwaa la mtandaoni la OnlyFans hadi klabu anayoshabikia itimue kocha wake.
Mwanamitindo huyo wa zamani amekiri kukerwa sana na matokeo duni ya timu yake ya O’Higgins inayoshiriki Ligi Kuu ya Chile.
Klabu hiyo kwa sasa inashikilia nafasi ya tisa kwenye jedwali la Ligi Kuu baada ya mechi saba.
Hiyo ni baada ya kushinda michuano mitatu, kusajili sare moja na kupoteza mechi tatu.
Isitoshe, ilibanduliwa kipute cha Copa Libertadores katika hatua ya mchujo na Tolima ya Colombia mabao 2-1.
Mnamo Jumatano, kipusa huyo alisema ataacha sasa kuburudisha mashabiki wake 20 milioni kwenye Instagram na X kwa picha na video za kuzingua, ikiwa vinara wa O’Higgins hawatafuata masharti yake.