Lugha, Fasihi na Elimu

Jinsi elimu ilivyoangaziwa katika riwaya ‘Nguu za Jadi’

Na JOYCE NEKESA, Kapsabet Boys April 9th, 2026 Kusoma ni dakika: 2

JUMA hili tutaangazia jinsi maudhui ya elimu yalivyoshughilikiwa katika riwaya ya ‘Nguu za Jadi’ tukirejelea swali lifuatalo la muktadha au dondoo.

“Hapo umesema ndugu. Na mia ka katika maisha hutufunza mengi kuliko hata hivyo vitabu. Ama kweli, elimu ni maisha si vitabu…”

(a) Eleza muktadha wa dondoo hili.

Msemaji – Mashauri.

Msemewa – Ngoswe.

Mahali – Ofisini mwa Mashauri.

Kiini – Ni baada ya Ngoswe kum julisha Mashauri kuwa Sagilu alikuwa pia babake wa kumzaa ndiposa wakatambua kuwa maisha ni mfuatano wa mafunzo ambayo mtu hana budi kuyaishi ili kuyaelewa.

(b) Jadili suala elimu lilivyoshuguliki wa na mwandishi wa riwaya.

Mwandishi anaithamini elimu ya maisha kuliko ya vitabuni kwa sababu ya changamoto ambazo waja wanakabiliana nazo ambazo huhitaji maarifa yanayopatikana kwa kuyaishi maisha yenyewe ili kuyaelewa.

Kwa kujadili suala la elimu, tutaangazia umuhimu wa elimu na changamoto zinazoikumba.

Ajira – Elimu husaidia mtu kupata kazi. Mangwasha alipata kazi ya uhazili katika ofisi ya Chifu Mshabaha kwa sababu alikuwa na vyeti alivyovithamini na kusema kuwa ndivyo vingemhakikishia ajira iwapo chifu angeamua kum timua kazini. (Uk. 3).

Pia elimu ya Mashauri ilimwezesha kuajiriwa kama msanifu wa majengo naye Cheiya akaajiriwa katika zahanati moja mjini Taria baada ya kufuzu katika taaluma ya uuguzi. (Uk. 117).

Ni silaha dhidi ya unyanyasaji – Lonare aliitumia elimu aliyopata kuwa silaha dhidi ya ubaguzi wa kika bila kwenye ajira.

Alipogundua kuwa mtemi alikataa kuwaajiri Waketwa, aliamua kuwapeleka wanawe ng’am bo ili wasomee taaluma mbalimbali (Uk. 50).

Mangwasha pia alitumia elimu yake kuwatetea Waketwa na kupinga maovu yaliyoendelezwa katika ofisi ya Chifu Mshabaha.

Husaidia kutoa maamuzi bora – Mangwasha alipewa elimumapokeo iliyompa mwongozo wa kukabili ugumu wa maisha na kufanya maamuzi mazuri.

Elimu huleta usawa palipokuwepo na elimu ya jinsia zote. Mrima na Mangwasha walipokea elimu. Pia Lonare aliwapeleka wanawe wa kiume na kike shuleni bila kubaguliwa.

Elimu pia imeangaziwa kuwa na changamoto zifuatazo:

Baadhi ya vijana waliohitimu kwenye taaluma mbalimbali wanapokosa kazi, wanashikilia kuwa elimu haina thamani. (Uk. 44).

Ukosefu wa elimu ya kutosha katika taaluma huleta maangamizi. Kwa mfano, karani walipoajiriwa kama daktari, walisababisha vifo vya kiholela hospitalini nao marubani walio na elimu duni wakasababisha ajali za ndege. (Uk. 44).

Viwango vya elimu vime shuka. Vilishuka kwani walimu walioajiriwa katika shule mbalimbali hawakuhitimu kwa masomo waliyoyafundisha na hivyo pakawa na bora elimu badala ya elimu bora. (Uk. 44).

Gharama ya juu ya elimu inasaba bisha watoto wa maskini kukatiza masomo na kuzurura ovyo kwenye mabaraste.

Tanbihi: Jadili namna ambavyo mrejelewa wa dondoo hili alivyoendeleza ploti ya riwaya.