Papa Leo aanza ziara Afrika, saa chache baada ya kuvurugana na Trump kuhusu Iran
KIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani Papa Leo XIV Jumatatu asubuhi aliondoka Roma kuelekea jijini Algiers nchini Algeria, kituo cha kwanza cha ziara yake ya siku 11 katika mataifa kadhaa ya bara Afrika.
Hiyo ni ziara yake ya kwanza kimataifa baada ya kuchaguliwa katika wadhifa huo na ziara ya kwanza Papa kufanya nchini Algeria, taifa ambako idadi kubwa ya raia ni Waislamu.
Kulingana na Askofu wa Kanisa Katoliki jijini Algiers, ziara ya Papa Leo inalenga “kujenga mahusiano katika ya Wakristo na Waislamu ulimwenguni.”
Kabla ya kukutana na Rais Abdelmadjid Tebboune na kuwahutubia maafisa wakuu wa serikali na wanadiplomasia, Papa huyo atatoa heshima zake kwa wahanga wa vita vya uhuru nchini Algeria vya kati ya 1954 na 1962 dhidi ya Ufaransa katika eneo la Ukumbusho wao jijini Algiers.
Kabla ya Papa Leo kutua Algiers kwa ziara hiyo ya kihistoria, kuta za majengo zimepakwa rangi upya, barabara zimesakafiwa upya na maeneo ya wazi wamerembeshwa kwa mimea na nyungu zenye maua ya kupendekeza.
Kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki pia atazuru mataifa ya Cameroon, Angola na Equatorial Guniea kabla ya kurejea nyumbani mnamo Aprili.
Ziara ya Papa Leo inajiri wakati mbapo vita vinaendelea katika eneo la Mashariki ya Kati na dalili zinaonyesha kuwa havitakoma hivyo karibuni baada ya Amerika na Iran kufeli kufikia makubaliano kwenye mazungumzo yaliyofanyika jijini Islamabad, Pakistan, Jumamosi.
Mnamo Jumamosi, katika hotuba katika Kanisa la St Peter’s Basilica, Leo alitoa wito kwa pande husika kusitisha vita hivyo.