Dondoo

Kizaazaa sokoni demu akizuia mume kupiga bei mbuzi wake

Na BENSON MATHEKA April 14th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

KITHYOKO, Kitui: 

JOMBI mmoja alijipata kona mbaya kwa kuiba mbuzi wa mkewe akauze ili alipe mkopo.

Inasemekana mwanamke huyo alimfuata mumewe hadi sokoni na kumtaka awarudishe mbuzi hao mara moja.

Jamaa huyo alikuwa amechukua mbuzi hao bila idhini ya mkewe, akafululiza hadi sokoni kuwauzaBaada ya jamaa kufika sokoni, alipigwa na mshangao kumuona mkewe katika soko.

“Rudisha mbuzi wangu nyumbani,” mkewe alifoka. Wanunuzi wa mbuzi hao walibaki midomo wazi wasijue la kumuambia jamaa.

“Nani alikupatia ruhusa ya kuleta mbuzi wangu sokoni? Kama unavuta bangi iache. Hii ni mali yangu,” mwanadada alimzomea mkewe.

Inasemekana mwanadada alichukua mbuzi wake na kuwaelekeza hadi nyumbani.

“Hii ni mali yangu, jasho langu. Wewe ni mzembe. Tafuta mbuzi wako uuze,” mwanadada aliendelea kumzomea mumewe.

Jamaa huyo, aliamua kuondoka katikati ya watu aibu ikimwandama.