Dondoo

Kalameni atimua barobaro mzungu kwa kubusu mkewe

Na KALUME KAZUNGU May 4th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

MUYEYE, Malindi:

BUDA mmoja kutoka majuu alijipata mashakani baba mkwe alipomwamuru kuondoka nyumbani mara moja akishuku kwa kumezea mate mkewe.

Inasemekana kijana huyo mzungu alikuwa amewatembelea jamaa akiandamana na binti yake waliyekuwa na nia ya kufunga pingu za maisha.

Binti alikuwa amemfikisha nyumbani ili kumtambulisha kwa wazazi wake kwa mara ya kwanza.

Jombi alionekana kuvutiwa mno na kumchangamkia mama mkwe mtarajiwa.

Mambo yaliharibika alipomshika na kumvuta karibu kabla ya kumpiga pambaja huku akimbusu kitendo kilichomkasirisha mzee wa boma akamwamuru jamaa aondoke mara moja nyumbani kwake.

“Umefika hapa kutujulisha nia ya kumuoa binti yangu ama umekuja kunipokonya mke wangu wewe. Achana na mke wangu, ondoka hapa. Sikutaki,” akasema buda huku akimwashiria mgeni huyo njia ya kuondoka bomani.