Habari

Nyanya zageuka bidhaa za ‘matajiri’ moja ikiongezeka hadi Sh25 ndani ya wiki mbili

Na JACKSON NGARI May 4th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

WAKENYA wengi sasa wameshindwa kumudu bei ya nyanya ambayo imepanda kwenye masoko mbalimbali jijini Nairobi

Uchunguzi uliofanywa na Taifa Leo katika masoko makubwa umeonyesha kuwa bei ya nyanya imefikia hadi Sh25 kwa nyanya mmoja, hali inayochochewa na gharama ya juu ya uzalishaji pamoja na ongezeko la mahitaji kutoka nchi jirani.

Wafanyabiashara wanasema bei ya jumla ya kreti moja ya nyanya imeongezeka maradufu katika miezi ya hivi karibuni. Hali hii imepunguza faida na kuwalazimu baadhi ya wanunuzi kununua nyanya zilizoharibika kidogo.

Awali nyanya ambazo zimeharibika kidogo zilikuwa zikitupwa katika masoko kama Soko la Wakulima na Soko la Kawangware.

“Hapo awali, kreti moja ilikuwa ikiuzwa kati ya Sh7,000 hadi Sh9,000, lakini sasa tunazinunua kwa Sh18,000 hadi Sh20,000,” akasema Vivian Wanjiru, mfanyabiashara wa kuuza nyanya Kawangware.