Madaraka Dei 2026: Maadhimisho ya miaka 63 ya utawala wa ndani kwa ndani
RAIS William Ruto leo, Jumatatu, Juni 1, 2026 anaongoza taifa kuadhimisha miaka 63 ya Kenya kujitawala kutoka mikononi mwa mbeberu.
Miongo sita na miaka mitatu iliyopita, Jamhuri ya Kenya ilipata uhuru wa ndani kwa ndani kujitawala chini ya Rais wa Kwanza hayati Mzee Jomo Kenyatta, ambaye kwa ushirikiano na vuguvugu la MauMau waliondoa utawala wa Muingereza.
Wakati huo, Juni 1, 1963, Mzee Jomo Kenyatta ambaye ni babake Rais mstaafu Uhuru Kenyatta, alihudumu kama Waziri Mkuu.
Maadhimisho ya miaka 63 yanafanyika katika uwanja wa Wajir, yakiongozwa na Rais Ruto, aliyeandamana pia na naibu wake Prof Kithure Kindiki na viongozi wengine wakuu serikalini. Hufanyika kila mwaka Juni 1.
Zifuatazo ni picha za hafla hiyo inayoendelea;









