Dimba

Trisha Khalid ajuta kutoka kimapenzi na mume wa mtu aliyempa gari la kifahari na maisha mazuri

Na SINDA MATIKO July 27th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

MWIGIZAJI staa Trisha Khalid anasema kuwa moja kati ya majuto makubwa aliyowahi kufanya ni kutoka kimapenzi na mume wa mtu.

Trisha amekiri kwamba pamoja na kwamba anajutia, mume huyo wa mtu alimpa maisha ya kifahari ikiwemo kumpa zawadi ya gari ya kifahari ya Mercedes Benz.

“Gari langu ya kwanza mimi kuimiliki nilipewa kama zawadi na ex wangu huyo aliyekuwa ni mume wa mtu. Ndio kwa kipindi kile niliona naishi maisha fulani hivi ila nilikuwa nakosea,” akasema Trisha.

Aidha mwigizaji huyo kaomba radhi akisema kuwa kila mtu hukosea na yeye kwenye hilo hakuchukua uamuzi sahihi.

“Naomba sana watu wasinihukumu, sote tunapitia vipindi vya kuteleza na kukosea. kipindi kile nilikuwa mdogo sijapevuka na nilikuwa naatamani maisha mazuri ambayo mwisho wa siku sikuyapata.”

Kulingana na Trisha, yule bwana mwishowe alikuja kuchukua gari lake walipogombana.

“Baada ya mimi kuona yale mahusiano hayakudumu, niliamua kumrejesha gari lake maana nilijua hakuwa ameandika kwenye jina langu na niliogopa aje kuitumia dhidi yangu. Na kwa sababu sipendi aibu na ninapenda kujiheshimu niliamua kumrudishia gari lake kabla hata hajaliomba,” akafunguka Trisha.