Habari

NMG yafanya mabadiliko katika uongozi wa uhariri

Na PATRICK LANG’AT September 16th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

NATION Media Group (NMG) imefanya mabadiliko katika uongozi wa uhariri yanayolenga kuimarisha ushirikiano katika vyumba vya habari na kukuza biashara zake za kikanda nchini Uganda na Tanzania.

Mabadiliko hayo yaliyotangazwa Jumatano na Mkurugenzi Mkuu na Afisa Mkuu Mtendaji Geoffrey Odundo pia yanalenga kuharakisha mabadiliko ya kidijitali katika shughuli za kampuni hiyo katika ukanda huo.

Mhariri Mkuu Msimamizi wa NMG, Dkt Joe Ageyo, amehamishiwa Uganda kushikilia wadhifa huo huo katika NMG Uganda.

Ataandamana na Washington Gikunju, ambaye ni Mhariri Msimamizi, Uchapishaji, Kenya, ambaye sasa atashikilia wadhifa huo NMG Uganda.

Nchini Kenya, Harry Misiko, ambaye alikuwa Mhariri Msimamizi anayesimamia Mikakati ya Maudhui, sasa ataongoza shughuli za chumba cha habari kama Kaimu Mhariri Mkuu Msimamizi.