• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 1:14 PM
Ashangaza kujificha msituni miaka 10 kuhepa ukorofi wa mkewe

Ashangaza kujificha msituni miaka 10 kuhepa ukorofi wa mkewe

MASHIRIKA Na PETER MBURU

MWANAMUME kutoka Uingereza ameshangaza ulimwengu baada ya kuibuka kuwa wakati fulani alipochoshwa na usumbufu wa mkewe, aliamua kwenda kwenye msitu kukaa huko, na akaishia kuishi mwituni kwa miaka 10.

Malcolm Applegate wa miaka 62 na ambaye alikuwa mfanyakazi wa shambani alikuwa amemwoa mkewe kwa miaka mitatu, wakati alipogundua kuwa usumbufu wake unazidi.

“Miaka mitatu ya kwanza mambo yalikuwa shwari, tulikuwa tukiishi vyema na inaonekana kazi yangu ya ukulima ikawa inamtatiza. Kadri nilivyozidi kufanya kazi, naye alikuwa akikasirika kwani hakupenda niwe nje ya boma kwa muda mrefu,” Applegate akaeleza Mashirika.

“Tabia yake ya kutaka kunidhibiti ilizidi na akaanza kunitaka nipunguze saa za kazi,” akaendelea.

Mwanamume huyo alisema ilipofika hapo, aliamua kuondoka katika boma lao na akaamua kuwa hangemfahamisha yeyote kilichokuwa katika akili zake, hata familia na marafiki.

“Niliwatoroka kwa muda wa miaka kumi,” akasema Applegate.

Alisema alitumia wiki tatu kutembea kutoka eneo la Oxford hadi London, ambapo alienda katika msitu mkubwa karibu na eneo la Kingston, kusini magharibi mwa Jiji la London.

Alisema humo alifanya kazi katika eneo la jamii, ambapo wazee wakongwe hukaa.

Applegate alisema katika eneo hilo ambapo alitorokea, kulikuwa na watu wengine ambao walikuwa wamepiga kambi na japo kila mmoja wao alikuwa akifanya kazi kivyake, mara kwa mara wangepatana katika eneo hilo palipokuwa pakiishi wazee, kwani walikuwa wakienda huko kuoga.

“Hakuna aliyejua kuwa tulikuwa huko kwani ni mahali pasipojulikana vyema- hakuna mtu angeenda huko ndani,” akasema.

Mwanamume huyo sasa anasema kuwa anaishi katika eneo pa watu wasio na makao, ambapo anafanya kazi za vibarua vibarua na anachangisha pesa za msaada eneo hilo.

You can share this post!

Abiria atolewa kwa ndege baada ya kuiombea ipate ajali

MKASA WA ETHIOPIA: Ruto, Mudavadi na Maraga watuma risala...

adminleo