• Nairobi
  • Last Updated March 19th, 2024 5:55 AM
Shujaa yakutanishwa na wakali Fiji na Samoa London Sevens

Shujaa yakutanishwa na wakali Fiji na Samoa London Sevens

Na GEOFFREY ANENE

DROO ya duru ya tisa ya Raga ya Dunia itakayofanyika jijini London nchini Uingereza mnamo Mei 25-26, 2019, imetangazwa, huku Kenya ikitiwa Kundi B pamoja na Fiji, Samoa na Ufaransa.

Shirikisho la Raga Duniani World Rugby limefanya droo hiyo baada ya duru ya nane kukamilika nchini Singapore mnamo Aprili 14.

Limekutanisha Afrika Kusini, Argentina, Canada na Japan katika Kundi A, Uingereza, New Zealand, Scotland na timu alikwa katika Kundi C nazo Marekani, Australia, Wales na Uhispania zinaunda Kundi D.

Kenya, Wales na Japan zinashikilia nafasi tatu za mwisho kwenye Raga ya Dunia ya msimu huu wa 2018-2019 zikikaribiana sana kwa alama baada ya kuzoa alama 26, 25 na 22 mtawalia katika duru nane za kwanza.

Timu hizi tatu ziko katika vita vikali vya kuepuka kumaliza msimu katika nafasi ya 15, ambayo atakayeishikilia baada ya duru ya mwisho nchini Ufaransa mnamo Juni 1-2 ataondolewa kwenye ligi hii ya kifahari.

Shujaa ya Kenya, ambayo msimu uliopita wa 2017-2018 ilijiandikia historia ya kuzoa zaidi ya alama 100, ilipata 104, itakuwa na kibarua kigumu katika kundi lake hasa kutokana na kwamba ina rekodi mbaya sana dhidi ya Fiji, Samoa na Ufaransa.

JEDWALI LA SINGAPORE SEVENS

Taifa   Alama

Afrika Kusini 22

Fiji 19

Uingereza 17

Marekani 15

Samoa 13

New Zealand 12

Argentina 10

Australia 10

Ufaransa 8

Scotland 7

Canada 5

Wales 5

Kenya 3

Uhispania 2

Hong Kong 1

Japan 1

MSIMAMO WA RAGA YA DUNIA 2018-2019:

Taifa   alama

Marekani  145

Fiji 142

New Zealand 130

Afrika Kusini 121

Uingereza 107

Samoa 87

Australia 80

Argentina 79

Ufaransa 71

Scotland 62

Uhispania 47

Canada 41

Kenya 26

Wales 25

Japan 22

You can share this post!

Idadi ya mabao itaamua watakaotinga Nne-bora –...

Kenya yaumizwa 2-0 na Morocco soka ya UNAF Misri

adminleo