• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Pendekezo magari ya masafa marefu yawe na madereva wawili

Pendekezo magari ya masafa marefu yawe na madereva wawili

Na BERNARDINE MUTANU

Pendekezo limetolewa ili magari ya umma yawe na madereva wawili ikiwa yanasafiri mwendo mrefu, zaidi ya kilomita 500.

Magari yanayoendeshwa kwa zaidi ya saa nane yanalengwa katika pendekezo hilo linalolenga kudhibiti idadi kubwa ya ajali za barabarani.

Ikiwa hakuna madereva wawili, dereva wa gari la masafa marefu anafaa kusimama kwa muda, baada ya kuwa barabarani kwa saa nyingi, kulingana na pendekezo hilo.

Pendekezo hilo lilitolewa na Shirika la Uchukuzi na Usalama barabarani (NTSA) katika notisi rasmi iliyochapishwa Januari 11.

Pendekezo hilo lilitolewa baada ya mamia ya Wakenya kuangamia katika ajali za barabarani hasa katika mwezi wa Desemba.

Ajali hizo zilisemekana kusababishwa na madereva wachovu na kuzembea kwa madereva. Kulingana na taratibu zilizopo, madereva wanafaa kuwa wawili usiku katika uchukuzi wa abiria kwa masafa marefu.

Kulingana na pendekezo jipya, madereva wanafaa kupumzika katika muda wa lisali moja baada ya kuendesha gari kwa saa nne.

You can share this post!

Mzigo wa deni la nchi sasa wavuka Sh4.5 trilioni

Fazul abana sababu ya kujiuzulu

adminleo