• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 10:55 AM
Waumini wa ACK wakataa uteuzi wa viongozi wapya jimbo la Kitale

Waumini wa ACK wakataa uteuzi wa viongozi wapya jimbo la Kitale

Na OSCAR KAKAI?

MZOZO katika kanisa la Anglikana katika kaunti ya Pokot Magharibi unaendelea kutokota huku baadhi ya waumini wakipinga viongozi wapya kwa madai ya uongozi mbaya.

Haya yanajiri siku tatu baada ya kanisa la ACK kumteua Dkt Emanuel Chemetich kuwa kasisi wa jimbo la Kitale mwaka jana.? Kwa zaidi ya miaka 25, kumekuwa na mizozo hiyo na kuchangia mgawanyiko kati ya wakristo katika kanisa hilo.

Mwaka jana, dayosisi ya Kitale iligawanyika kutokana na mizozo kati ya waumini wa kanisa hilo huku zaidi ya waumini elfu kumi kutoka kaunti ya Pokot Magharibi wakiamua kujiondoa kutoka kwenye dayosisi hiyo.

Baadhi ya wakristo hao kutoka kaunti ndogo zote nne katika kaunti ya Pokot Magharibi walijiondoa kutoka dayosisi ya Kitale na kuzindua rasmi dayosisi ya Kapenguria na kuanza shughuli zao wakiwasiliana na eneo la mkoa chini ya askofu mkuu wa kanisa hilo nchini, Jackson Ole Sapit.

Mizozo hiyo imeleta migawanyiko kati ya wakristo na hata kulemaza shughuli za dayosisi asili ya Kitale.

Wakiongea na wanahabari mjini Kapenguria, Wakristo hao walipinga askofu Chemetich kuwa aliteuliwa bila kufuata utaratabu na kumtaka askofu mkuu kuwapa dayosisi.?Kundi moja linataka kubuniwa kwa dayosisi mpya ya Kapenguria huku jingine likitaka kusalia ile ya Kitale.

Mzozo wa uongozi kati ya waumini umeendelea kushuhudiwa huku wakristo zaidi ya elfu kumi wakijiondoa kutoka kwa dayosisi ya Kitale na kuzindua rasmi doyosisi ya Kapenguria na kuanza shughuli zao wakiwasiliana na eneo la mkoa chini ya askofu mkuu wa kanisa hilo nchini, Jackson Ole Sapit.

You can share this post!

Shule zafunguliwa mtaala mpya ukitekelezwa

Polisi wasaka genge hatari linalohusishwa na wanasiasa

adminleo