• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:00 PM
Wakazi wamtaka Waititu awape huduma bora

Wakazi wamtaka Waititu awape huduma bora

Na LAWRENCE ONGARO

WAKAZI wa Thika wameikejeli serikali ya Kaunti ya Kiambu kwa kuzembea katika utendakazi wake katika kile wanachoamini ni kupuuzwa na usimamizi wa kaunti.

Wakiongozwa na mwenyekiti wa wafanyabiashara Bw Alfred Wanyoike, walisema mashimo mengi ya maji taka yameachwa wazi jambo ambalo ni hatari kwa usalama kwa wapitanjia na wenye magari.

“Sisi kama wakazi wa eneo hilo tumebaki tukijiuliza kama kweli tuna viongozi. Haya mashimo ya maji taka yanatuweka na wasiwasi mwingi,” alisema Bw Wanyoike.

Alisema hivi majuzi mwanamke mmoja mjamzito alivujika miguu akijaribu kuruka mojawapo ya mashimo  ambapo aliumia vibaya.

Alifafanua kuwa mahali mambo yamefika sio kuulizia kutendewa kazi bali ni kuwalazimisha kimambavu  kwa sababu wanatoa kodi ya huduma.

Iwapo watazidi kuzembea kazini wananchi wameapa kuwashurutisha wahusika kufanya kazi hiyo.

 

“Tutaandamana ili kuonyesha ghadhabu zetu kwa serikali ya Kaunti ya Kiambu, inayoongozwa na Bw Ferdinand Waititu,” alisema Bw Wanyoike.

Baadhi ya maeneo yaliyoathirika kwa kupata mashimo hayo ni barabara Za Uhuru, Mama Ngina, Nkrumah, na Kenyatta.

 

You can share this post!

IEBC yajitetea kuhusu matumizi ya Sh690m kwa mapochopocho

Suarez awakejeli wenzake kuaibishwa na Liverpool

adminleo