• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 6:50 PM
Utulivu warejea Burkina Faso baada ya shambulio la kigaidi

Utulivu warejea Burkina Faso baada ya shambulio la kigaidi

Ouagadougou, Burkina Faso

SHUGHULI za kibiashara zilirejea katika soko kuu la jiji kuu la Burkina Faso, Ouagadougou Jumamosi siku moja baada ya magaidi wa Kiislamu kushambulia Ubalozi wa Ufaransa na makao makuu ya kijeshi ambapo watu wanane waliuawa na wengine 80 wakajeruhiwa.

Kundi linaloshirikiana na mtandao wa Al Qaeda la The Group to Support Islam and Muslims (GSIM) lilikiri lilitekeleza shambulio hilo ambalo waziri mkuu alilitaja kama la watu waoga.

GSIM ilisema shambulio hilo lilikuwa la kulipiza kisasi mauaji ya baadhi ya viongozi wake na jeshi la Ufaransa wiki mbili zilizopita Kaskazini mwa Mali. Uchunguzi unaendelea kuhusu shambulio hilo.

Watu walirejea katika barabara za jiji hilo. Wanajeshi waliwaua magaidi wanane na watu kadhaa walikamatwa. Harufu ya moshi ilitanda katika jiji hilo Jumamosi.

Shimo kubwa kwenye uwanja wa makao hayo na alama kwenye ukuta zilidhihisha jinsi magaidi waliovalia sare walilipua bomu kwenye gari wakilenga chumba ambacho maafisa wakuu wa jeshi walipaswa kukutana lakini wakaamua kukutana eneo tofauti kulingana na maelezo ya waziri wa usalama Clemement Sawangongo.

Chumba hicho kiliharibiwa kabisa na vipande vya magari kutapakaa kote ndani ya makao makuu ya jeshi. Sawadogo alisema kuwa iwapo mkutano usingefanyika katika chumba tofauti, jeshi lisingesalia na wakubwa. Mwanajeshi mstaafu Amado Belem aliambia shirika la habari la Associated Press kwamba hakufurahishwa na shambulio hilo.

“Inashtusha kuona jeshi likishambuliwa rahisi hivi”, alisema.

 

Mara ya tatu

Hii ilikuwa mara ya tatu ya magaidi wa Kiislamu kushambulia jiji hilo tangu Januari 2016 na kufanya jeshi kulaumiwa. Kufikia Jumamosi hakuna kundi lililojitokeza kudai lilitekeleza shambulio hilo.

Watu walijazana karibu na makao makuu ya jeshi na Ubalozi wa Ufaranza kutazama uharibifu huo. Mabaki ya gari lililochomeka yalikuwa nje ya Ubalozi huo uliojaa mashimo ya risasi ukutani.

Ubalozi huo ulishambuliwa saa nne na robo Ijumaa huku watu waliokuwa ofisi jirani za kituo cha runinga cha serikali wakisema washambuliaji walifika wakibebwa na lori mdogo wakiimba Allahu Akbar na kuanza kufyatua risasi.

Hakuna aliyejeruhiwa katika Ubalozi huo lakini mlinzi mmoja na washambuliaji wanne waliuawa, waziri wa mashauri ya kigeni wa Ufaransa Jean-Yves Le Drian alisema kwenye ujumbe uliopeperushwa kupitia runinga.

Wakazi walisema wanahofia usalama wao kufuatia shambulio hilo. “Hali ni mbaya sana. Unaona, tulidhani ni vitoa machozi vilivyokuwa vikilipuliwa kutoka ubalozi wa Ufaranza lakini ilikuwa ni risasi halisi zilizoua watu.

Watu walikimbia hadi ofisi ya waziri mkuu. Ilikuwa hivi siku nzima ,” alisema Sylvain Some, anayefanya kazi kwenye kibanda karibu na Ubalozi huo. GSM limekuwa likitekeleza mashambulio mali.

You can share this post!

SHANGAZI AKUJIBU: Mume wangu bado anafuatafuata mke wa...

NYOTA YAKO: MACHI 5, 2018

adminleo