• Nairobi
  • Last Updated April 23rd, 2024 9:40 PM
TZ mbioni kuokoa wavuvi wake waliokamatwa na maafisa wa Kenya

TZ mbioni kuokoa wavuvi wake waliokamatwa na maafisa wa Kenya

NA WINNIE ATIENO

SERIKALI ya Tanzania imeingilia kati kesi kuhusu raia wake wapatao 108 waliokamatwa na maafisa wa huduma za kulinda Pwani ya Kenya.

Serikali ya Rais John Magufuli imewahakikishia raia wake waliokuwa wakivua samaki katika Bahari Hindi sehemu ya Kenya walipozuiliwa na maafisa wa Kenya baada ya kupatikana bila vibali, kwamba watarudishwa nyumbani.

Wavuvi hao walikamatwa baada ya vyombo vyao 23 vya uvuvi kupatikana Kilifi, Wesa, Watamu, Ngomeni, Malindi, Uyombo, Mayungu na eneo la Kipini mnamo Ijumaa.

Wavuvi hao aidha walisema walipatikana humu nchini baada ya kusombwa na mawimbi makali kufuatia baridi ya kusi.

Lakini halmashauri ya huduma za kulinda bahari ya Kenya ilisema baadhi ya wavuvi hao hawakuwa na vibali.

“Ninataka kuwashukuru wavuvi wa humu nchini na serikali ya kaunti ya Kilifi kwa kuwaokoa wavuvi wenzao wa Tanzania ambao walijipata humu nchini kufuatia hali mbaya ya hewa huku mvua ikiendelea kunyesha sehemu ya Pwani,” alisema afisa wa Balozi wa Tanzania nchini, Bw Athman Haji.

Bw Haji ambaye aliwatembelea raia hao siku ya Jumamosi alisema watasafirishwa nchini Tanzania lakini vyombo vyao vya uvuvi vitsalia humu nchini mpka hali ya anga itakapo badilika.

“Tutaangalia hali zao kabla ya kuwasafirisha Tanzania ambako mnasubiriwa, lakini vyombo vyenu vitabakia sababu ya hali ya anga bado ni mbaya, mtakapopata stakabadhi zinazohitajika mtarudi kuzichukua,” akasema Bw Haji alisema.

Jumamosi, Luteni Kamanda wa KCGS Glen Majanga alisema walipokea habari kuhusu boti 23 kutoka Pemba na watu 108 ndani mwao wakiyumbayumba sehemu ya fuo za Kenya upande wa Kilifi kufuatia hali mbaya ya anga.

You can share this post!

Magavana walia kuteswa na maseneta

SAKATA YA DHAHABU FEKI: Raila ajikaanga

adminleo