• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 12:30 PM
Kidosho pabaya kupapasa polo mbele ya majirani

Kidosho pabaya kupapasa polo mbele ya majirani

Na JOHN MUSYOKI

KATHIANI, MACHAKOS

KIDOSHO mmoja kutoka eneo hili, alijipata kona mbaya alipompapasa jamaa na kumbusu hadharani mbele ya wapangaji plotini.

Inasemekana demu huyo alikuwa akijipendekeza kwa jamaa huyo kwa muda mrefu lakini polo alimpuuza kwa sababu alikuwa akipenda pombe kupita kiasi.

Siku ya kioja demu alitoka kwa mama pima na kumpata jamaa akiwa ameketi nje ya chumba chake akipiga soga na majirani. Penyenye zinasema demu alianza kutabasamu kisha akamkaribia jamaa na kuanza kumpapasa kabla ya kumpa busu moto.

Inasemekana jamaa alianza kumfokea. “Shindwe kabisa kahaba wewe. Nani amekupa ruhusa ya kunikaribia na kunipapasa. Ona midomo yako michafu,” jamaa alisema huku akimtemea demu mate usoni.

Jamaa alipandwa na hamaki na kumwangushia demu kofi usoni. “Mimi sikupendi hata ukijipendekeza kwangu kiasi gani. Tabia yako siipendi hata kidogo.

Hauna maadili mema na siwezi kupoteza wakati wangu nikikutongoza.Toka mbele yangu ama nikuharibu sura, shetani wewe. Siku nyingine ukijaribu kunikaribia nitakuonyesha cha mtema kuni,” alisema.

Alitaka kumpokeza kichapo zaidi lakini alizuiliwa na wapangaji waliomwambia demu alikuwa amepata funzo.

You can share this post!

Kalameni aliyezaa na dada apanga kumuoa

Kioja mwizi wa pikipiki kuirejesha huku akilia

adminleo