• Nairobi
  • Last Updated April 23rd, 2024 10:10 AM
Wagonjwa KNH kuanza kuwekewa vibandiko

Wagonjwa KNH kuanza kuwekewa vibandiko

Na ELIZABETH MERAB

HOSPITALI Kuu ya Kenyatta (KNH) inatarajiwa kuhakikisha kuwa wagonjwa wote wanawekwa vibandiko vya majina yao muda wanapolazwa, na wakati wote wakiwa katika hospitali hiyo.

Hospitali hiyo pia inahitajika kuanza kutumia kalamu maalum kuweka alama kwa sehemu za upasuaji kwa wagonjwa wanaotarajia kufanyiwa upasuaji.

Ikitoa ripoti ya uchunguzi wa awali, bodi ya usimamizi ilipatia hospitali mapendekezo manne ambayo inatarajia yaketekelezwe.

Pia kutatua suala hilo, bodi hiyo inayoongozwa na Bw Mark Bor, ilisema kuwa imekamilisha na kuwasilisha ripoti ya uchunguzi wake wa awali kwa Wizara ya

Afya ikiwa na mapendekezo ya kuangaliwa upya kwa saa za kufanya kazi na utaratibu wa kazi wa maafisa wa matibabu.

Kanuni hizo mpya zimefuatia tukio ambapo mgonjwa ambaye hakustahili kufanyiwa upasuaji, aliishia kufanyiwa upasuaji wa ubongo.

Tukio hilo lililotakana na hali ya mgonjwa aliyefanyiwa upasuaji kuwekwa kibandiko cha jina ambalo halikuwa lake.

Madaktari walisema kuwa hawakugundua kosa hilo hadi saa kadha upasuaji ukiendelea walipogundua hakukuwa na damu iliyoganda kwa ubongo wa mwanamume huyo.

Jumamosi, bodi hiyo pia ilitangaza kuwa imeondoa agizo la kusimamishwa kazi kwa daktari, afisa wa masuala ya matibabu na wauguzi wawili ili kutoa nafasi ya chunguzi huru kufanywa kuhusiana na tukio hilo.

 

You can share this post!

KIFO CHA NASA: Dalili zote za muungano kusambaratika

Joho awapongeza Raila na Uhuru

adminleo