• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 9:15 PM
Polisi lawamani kwa kuteketeza nyumba tisa

Polisi lawamani kwa kuteketeza nyumba tisa

Na CHARLES WANYORO

POLISI katika eneo la Igembe Kusini, Kaunti ya Meru, wamekosolewa vikali kwa madai ya kuchoma nyumba tisa kijijini Thunu, Kaunti Ndogo ya Igembe Kusini.

Wakazi waliopiga kambi katika kanisa la Christ Gospel Mission walisema takriban maafisa 40 wa polisi walivamia eneo hilo mnamo Jumamosi na kupiga risasi hewani kabla ya kuzitia moto nyumba hizo na kusababisha uharibifu mkubwa.

Bi Jane Kaari, 46, mkazi, alieleza jinsi maafisa hao waliokuwa wameandamana na wasimamizi wa eneo hilo (chifu na msaidizi wake) walivyofika mwendo wa saa sita mchana walipokuwa wakitayarisha maakuli ya mchana na kuanza kufyatua hewani.

Alisema maafisa hao walionekana kulenga nyumba fulani kwani walionyesha nyumba zilizofaa kuharibiwa kabla ya kuzivunja na kuzitia moto.

“Walisema walikuwa wamewasili kwa nyumba zilizolengwa kabla ya kuanza kutoa maagizo. Nilitazama mbuzi, vyakula na kuku wakichomeka. Walisema walikuwa wakifukuza wahalifu. Tumefanya nini sisi? Hatuna haki? Tunahisi kubaguliwa,” alisema.

Alieleza kuwa kulikuwa na mzozo kuhusiana na kipande cha ardhi cha ekari 50 na huenda kilikuwa sababu ya kuchomwa kwa nyumba zao, kwa kulenga kuwahofisha wakazi.

You can share this post!

Pigo jipya kwa juhudi za IEBC kuteua mrithi wa Chiloba

Nipeni ruhusa nipatanishe Mlima Kenya – Waiguru

adminleo