• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 10:50 AM
Trump ampiga kalamu Rex Tillerson akiwa Afrika

Trump ampiga kalamu Rex Tillerson akiwa Afrika

Na BENSON MATHEKA

RAIS wa Amerika, Donald Trump alimfuta kazi waziri wake wa mashauri ya nchi za kigeni, Rex Tillerson, siku moja baada ya kuzuru Kenya.

Mnamo Jumatatu, Bw Tillerson alikatiza ziara yake barani Afrika na kurudi Amerika katika kile kilichotajwa kama kushughulikia masuala ya dharura.

Kwenye ujumbe wa Twitter punde tu baada ya Bw Tillerson kurejea Amerika, Bw Trump alitangaza kwamba alikuwa amemteua Mkurugenzi wa shirika la ujasusi (CIA) Bw Mike Pompeo kuwa waziri mpya wa mashauri ya kigeni.

“Mike Pompeo, Mkurugenzi wa CIA, atakuwa waziri wetu mpya wa mashauri ya nchi za kigeni. Atafanya kazi nzuri. Asante Rex Tillerson kwa huduma zako,” Trump alisema kwenye Twitter.

Bw Tillerson aliwasili Nairobi Ijumaa muda mfupi baada ya Rais Uhuru Kenyatta kukutana na hasimu wake wa kisiasa Raila Odinga.

Alikutana na kushauriana na Rais Kenyatta kabla ya kushauriana na waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Kenya, Dkt Monica Juma na mwenzake wa utalii Najib Balala.

Kwenye kikao na wanahabari jijini Nairobi, alisema alifurahishwa na mkutano wa Rais Uhuru na Bw Odinga akitaja hatua hiyo kuwa muhimu kukuza uwiano nchini.

Mnamo Jumamosi, alipangiwa kuhudhuria kikao pamoja na waziri wa afya Sicily Kariuki katika hospitali ya Pumwani lakini kilifutiliwa mbali dakika za mwisho ikisemekana alikuwa ameugua. Alitarajiwa kuzuru Somalia lakini akafutilia mbali ziara hiyo.

Aliondoka Kenya Jumatatu kuelekea Chad na Nigeria.

You can share this post!

Sakata mpya ya mahindi serikalini yawaletea wakulima hasara...

Mwanaume ajuta kumuua mwanawe na kusulubisha mwili kama Yesu

adminleo