• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 6:27 PM
Wahimizwa wasibague mahabusu wa zamani

Wahimizwa wasibague mahabusu wa zamani

Na ELIJAH MWANGI

WAKAZI wa Meru wametakiwa kukoma kuwabagua wafungwa wa zamani.

Machifu wawili; Bi Isabel Mutura wa lokesheni ya Kanyekine na Bi Mercy Mureithi wa lokesheni ya Municipality, Imenti Kaskazini, walisema wakazi wa eneo hilo wamekuwa na mazoea ya kuwabagua wafungwa wanaoachiliwa huru baada ya kukamilisha kifungo chao gerezani.

Bi Mutura alisema kutengwa kwa wafungwa hao wa zamani kunawasukuma kujiingiza kwenye uhalifu na hata kujitoa uhai kwani wanahisi kukataliwa na jamii.

“Wafungwa wa zamani wanachohitaji ni upendo na kusaidiwa kurejelea maisha yao ya awali,” akasema Bi Mutura.

Machifu hao walikuwa wakizungumza katika hafla ya mazishi ya mwanaume aliyejitia kitanzi kwa madai ya kukataliwa na mkewe na watoto wake wawili aliporejea nyumbani baada ya kukamilisha kifungo cha miaka mitano gerezani.

Inadaiwa familia ya mwanaume huyo iliuza shamba alipokuwa gerezani na kuhamia mjini.

Bi Murithi aliwataka wafungwa wanaotoka jela kujiunga na kikundi kilichobuniwa mnamo 2004 kuwasaidia wafungwa wanaorejea baada ya kukamilisha adhabu zao kutangamana na jamii.

“Wafungwa waliojiunga na kikundi hicho wanasaidiwa kuendelea na maisha yao ya hapo awali na kuhimizwa kuwa watu wema,” akasema.

You can share this post!

Viongozi wahimiza raia wajitokeze kwa sensa

KIKOLEZO: Ngoma ikichacha…

adminleo