• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 7:45 AM
Pigano la Okwiri na Ouma laahirishwa hadi Aprili 18

Pigano la Okwiri na Ouma laahirishwa hadi Aprili 18

Na GEOFFREY ANENE

PIGANO la kimataifa la uzani wa ‘welter’ kati ya Mkenya Rayton Okwiri na Mganda Kassim Ouma hapo Machi 30 limeahirishwa hadi Aprili 18, 2018.

Okwiri, ambaye anaishi na kufanyia mazoezi yake Marekani, alitangaza kubadilishwa kwa tarehe hiyo Machi 21 kupitia mtandao wake wa Facebook.

“Pigano langu, ambalo liliratibiwa kufanyika Machi 30 limesukumwa mbele hadi Aprili 18,” alisema Okwiri, ambaye siku chache zilizopita alikuwa ametangaza amejiandaa vyema na yuko tayari kutua jijini Nairobi kwa pambano hilo lililopangiwa kuandaliwa katika Jumba la Mikutano la KICC.

Okwiri na bingwa wa zamani wa taji la kimataifa la IBF, Ouma, walipangiwa kulimana katika pigano lisilo la taji, lakini muhimu sana.

“Ni pigano litakaloamua bondia atakayepata tiketi ya kuwania taji la dunia la WBA mwezi Juni. Pigano kati yangu na Ouma ni mechi ya kufuzu kushiriki pigano la Juni,” Okwiri aliambia Taifa Leo katika mahojiano ya kipekee kutoka Marekani.

You can share this post!

Utepetevu hospitalini KNH unavyomsababishia mama uchungu

Itawabidi Stars kujikakamua zaidi kuzima Comoros na CAR,...

adminleo