• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:42 PM
Wahariri waonya wanaodhuru wanahabari

Wahariri waonya wanaodhuru wanahabari

Na KALUME KAZUNGU

BODI ya wahariri wa Habari nchini (Editors Guild) imeonya vikali tabia ya baadhi ya watu kuwashambulia wanahabari wanapokuwa kazini.

Katika kikao kilichowakutanisha wananchi na wahariri hao kwenye ukumbi wa hoteli ya Mwana Arafa mjini Lamu Jumamosi, Rais wa bodi hiyo, Bw Churchill Otieno, alisema hawatamsaza yeyote atakayejaribu kuingilia au kuzuia utendakazi wa wanahabari kupitia kuwavamia na kuwapiga au kuharibu vifaa vyao vya kufanyia kazi.

Bw Otieno alisema kuwashambulia wanahabari ni sawa na kuushambulia umma, hivyo akasisitiza haja ya wenye nia hiyo mbovu kukoma.

Pia aliwataka viongozi na wakazi kuwa mstari wa mbele katika kudhibiti usalama wa wanahabari kwenye maeneo yao ili watekeleze jukumu lao la kuupasha umma habari ipasavyo na kwa wakati ufaao.

Katibu Mkuu wa Muungano wa kutetea Maslahi ya Wanahabari (KUJ), Bw Eric Oduor, alisema tayari wamehakikisha wote waliojaribu kuwashambulia wanahabari wanakamatwa na kufikishwa kortini hapa nchini.

Alitaja kisa cha kupigwa kwa mwanahabari wa gazeti la Standard anayefanya kazi Lamu, Bi Jane Wangechi Mugambi na Mwakilishi Maalum wa Bunge la Kaunti ya Lamu, Bi Monica Njambi, kuwa mojawapo ya mifano ambapo KUJ imehakikisha haki inatendeka kwa wanahabari wanaodhulumiwa nchini.

You can share this post!

Hakuna mzaha, maafisa wa KFS waanza kuingia Mau

Kenya Power kutumia Sh9.5b kuunganisha umeme Nyanza

adminleo