• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Kampuni 5 zanufaika na malipo ya chini forodhani

Kampuni 5 zanufaika na malipo ya chini forodhani

Na BERNARDINE MUTANU

KAMPUNI tano za Kenya zimepewa cheti cha kijamii, ambapo zitakuwa na uwezo wa kupokea huduma zaidi za forodhani kwa malipo ya chini.

Kampuni hizo: Isuzu East Africa Ltd, Kuehne Nagel Limited, Bollore Africa Logistics, Ufanisi Freighters Limited na Farmers Choice Limited zilipendekezwa na Shirika la Ukusanyaji Ushuru(KRA)kuwekwa katika orodha ya kampuni ambazo zinafaidika kutokana na huduma hiyo.

Kampuni hizo zilipokea vyeti vyao wakati wa mkutano wa nne wa mashirika ya forodha ulimwenguni (WCO) na mashirika ya kibiashara kati ya Machi 14 na Machi 16, 2018, Kampala, Uganda.

Mizigo ya mashirika yaliyo katika orodha hiyo itakuwa ikiachiliwa moja kwa moja forodhani, alisema Mkurugenzi Mkuu wa KRA John Njiraini wakati wa mkutano huo.

Kampuni hizo zimefikisha 14 idadi ya kampuni za Kenya ambazo zimepewa cheti hicho, kati ya kampuni 73 katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

You can share this post!

Waholanzi sasa ndio wateja wakuu wa bidhaa za Kenya

I&M pia yapungukiwa na faida

adminleo