• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 3:04 PM
MAPISHI: Jinsi unavyoweza kuandaa ‘fluffy pancakes’

MAPISHI: Jinsi unavyoweza kuandaa ‘fluffy pancakes’

Na MARGARET MAINA

[email protected]

Muda wa kuandaa: Dakika 10

Muda wa kupika: Dakika 15

Walaji: 5

Fluffy pancake. Picha/ Margaret Maina

Vinavyohitajika

  • unga wa ngano kilo ½
  • vijiko 3 vya sukari
  • kijiko ½ cha Baking Soda
  • kijiko ½ cha Baking Powder
  • kijiko ½ cha chumvi
  • mayai 2
  • kijiko 1 cha siagi
  • kijiko 1 cha vanilla
  • mafuta ya kupikia

Maelekezo

Chukua bakuli safi na kwalo – likiwa kavu – changanya unga wa ngano, sukari, chumvi, baking powder na baking soda.

Kisha chukua bakuli jingine safi na kavu kisha changanya pamoja mayai, vanilla essence, siagi na fresh cream. Kama huna, unaweza kutumia maziwa badala yake.

Mchanganyiko wa vinavyohitajika katika mapishi ya fluffy pancake. Picha/ Margaret Maina

Sasa chukua mchanganyiko wa mayai na maziwa umwagie kwenye mchanganyiko wa unga na halafu koroga polepole. Weka pembeni; acha kwa muda wa dakika tano. Si lazima lakini kama ukiweka kwa muda huo itulie, bila shaka pancake yako itatoka vizuri sana.

Chukua non stick pan, mimina mafuta kiasi na halafu hakikisha meko yako hayana moto mkali au moto mdogo.

Chukua kijiko kikubwa; chota mchanganyiko wako na mwagia katika kikaangio.

Pindua pancakes ikiwa rangi ya kahawia na uache iive upande mwingine.

Epua, pakua na ufurahie na chochote ukipendacho.

You can share this post!

Mwanamume, 51, akatwa sehemu nyeti na wenzake akiwa...

Uhuru wa wanahabari utiliwe mkazo Afrika – BBC

adminleo