• Nairobi
  • Last Updated April 23rd, 2024 9:40 PM
Uhuru wa wanahabari utiliwe mkazo Afrika – BBC

Uhuru wa wanahabari utiliwe mkazo Afrika – BBC

Na VALENTINE OBARA

SHIRIKA la kimataifa la habari la BBC, Jumatano lilitoa wito kwa mashirika mengine ya habari Afrika kutilia mkazo umuhimu wa uhuru wa kutekeleza wajibu wao bila ushawishi kutoka nje.

Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo Bw Tony Hall alisema uhuru wa vyombo vya habari ni nguzo muhimu katika kukomesha maovu barani na kutetea wanyonge katika jamii.

“Uhuru wa vyombo vya habari unahitajika sasa kuliko wakati mwingine wowote wa enzi zilizopita. Uhuru huu unazidi kukandamizwa. Kuna mataifa mengi ambayo yamepitisha sheria za kukandamiza vyombo vya habari. Haya ni masuala tunayohitaji kuwazia na kuweka pia mikakati ya kulinda wanahabari zaidi,” akasema.

Alikuwa akizungumza kwenye hafla iliyoleta pamoja wadau wa sekta ya vyombo vya habari Nairobi Jumatano usiku, akiwemo afisa mkuu mtendaji wa kampuni ya Nation Media Group, Bw Stephen Gitagama.

Wakati huo huo, shirika hilo lilitangaza mpango maalumu wa kusaidia wanahabari walemavu kupata nafasi ya kujistawisha katika taaluma zao.

Bw alisema mpango huo unaofahamika kama Aim High utatoa mafunzo kwa wanahabari walemavu kuanzia Aprili mwaka ujao.

Wale watakaofuzu kwa nafasi hizo watapewa nafasi kufanya kazi wakijinoa kitaaluma katika afisi za BBC zilizo Nairobi.

Nairobi ina afisi kubwa zaidi ya BBC barani Afrika baada ya makao makuu ya shirika hilo London, Uingereza.

Bw Hall alikuwa nchini kwa sherehe za shirika hilo kuhusu mafanikio yake barani Afrika ambako inatangaza habari kwa lugha 13 tofauti ikiwemo Kiswahili kupitia kwa runinga, redio na mitandao.

You can share this post!

MAPISHI: Jinsi unavyoweza kuandaa ‘fluffy...

Sababu ya Equity kuangusha benki zingine michezoni

adminleo