• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 7:50 AM
Mathare kuchupa juu ya Gor wakiilima Chemelil Sugar

Mathare kuchupa juu ya Gor wakiilima Chemelil Sugar

Na GEOFFREY ANENE

MATHARE United na Chemelil Sugar zitavaana Ijumaa, huku Ligi Kuu ya Soka ya Kenya ikiendelea baada ya kipindi cha siku 11 cha mechi za timu za taifa kukamilika.

Mabingwa wa mwaka 2008 Mathare, ambao wanashikilia nafasi ya nne, wana fursa murwa ya kujitosa juu ya jedwali la ligi hii ya klabu 18, wakipiga nambari saba Chemelil.

Mathare ya kocha Francis Kimanzi imezoa alama 14 kutoka mechi saba. Itaruka viongozi Gor Mahia, ambao wamevuna alama 16 kutoka mechi sita, nambari mbili AFC Leopards, ambayo pia imekusanya alama 16, lakini kutoka mechi saba, na nambari tatu Bandari, ambayo imevuna alama 14 kutoka mechi saba.

Wanasukari wa Chemelil watarukia nafasi ya nne na kusukuma Mathare, mabingwa wa mwaka 2009 Sofapaka, na Kariobangi Sharks nafasi moja chini kila mmoja wakilemea Mathare.

Hata hivyo, matokeo ya mechi kati ya klabu hizi inaonyesha kuna asilimia kubwa itaishia sare. Mechi 10 kati ya 12 zao za mwisho zimemalizika sare kwenye ligi.

Msimu uliopita, klabu hizi ziligawana pointi katika sare ya 0-0 Mathare ilipokuwa nyumbani Aprili 26 kabla ya kupiga sare ya 1-1 katika mechi ya marudiano Oktoba 1.

Mara ya mwisho Chemelil ilizaba Mathare ilikuwa 2-1 Agosti 16 mwaka 2014. Mathare ililipiza kisasi 1-0 Februari 21, 2016.

Kutokana na takwimu hizi ni wazi kwamba nambari nne Mathare na nambari saba Chemelil inatarajiwa kuwa ngumu.

Ratiba:

Machi 30

Mathare United vs. Chemelil Sugar (3pm, Machakos)

Machi 31

Posta Rangers vs. Thika United (2pm, Camp Toyoyo)

Kariobangi Sharks vs. Ulinzi Stars (4.15pm, Camp Toyoyo)

Kakamega Homeboyz vs. Bandari (3pm, Bukhungu)

Gor Mahia vs. Vihiga United (3pm, Kisumu)

Nzoia Sugar vs. SoNy Sugar (3pm, Sudi)

Nakumatt vs. Sofapaka (3pm, Ruaraka)

Aprili 2

Zoo vs. Wazito (2pm, Kericho)

Tusker vs. AFC Leopards (4.15pm, Kericho)

You can share this post!

Girona ya Olunga yaharamisha uvutaji sigara

Jeraha lapona, Cherop sasa kushiriki mbio za Rome Marathon

adminleo